Mechi mbili za hatua ya awali ligi ya mabingwa zimekamilika huku Yanga ikifanikiwa kutinga raundi ya kwanza kwa ushindi wa jumla wa mabao 3-2 dhidi ya Gaborone United.
Kilichowafurahisha mashabiki wa Yanga ni kuona washambuliaji wao wote watatu wanashiriki katika kuivusha Yanga kufuzu raundi ya kwanza.
Seleman Mwalimu ndiye aliyefunga bao la kusawazisha dakika za lala salama kwenye mchezo wa kwanza uliopigwa Botswana na kumalizika kwa matokeo ya sare ya bao 1-1.

Peter Shalulile juzi akaitanguliza Yanga kwa kufunga bao la kwanza dimba la Azam Complex akipokea pasi kutoka kwa Mwalimu kabla ya Cheick Ibrahim Toure kuongeza bao la pili kipindi cha pili.
Pengine Mwalimu angeweza kufunga tena katika mchezo huo lakini pasi yake ya bao ilikuwa muhimu.
Mpaka sasa washambuliaji wa Yanga wamehusika kwenye mabao 7 katika mashindano yote.
Shalulile anaongoza akiwa amefunga mabao manne (matatu kafunga kwenye ligi), Toure amefunga mabao mawili (moja kwenye ligi) na Mwalimu amepachika bao moja kwenye ligi ya mabingwa