Mabingwa watetezi wa ligi kuu ya NBC, Yanga Sc leo wanarudi kwenye kampeni ya kurejesha taji hilo Jangwani kwa msimu wa sita mfululizo pale watakapo wakaribisha Geita Gold katika mchezo utakaopigwa uwanja wa KMC Complex, saa 1 usiku.
Baada ya kufanikiwa kuvuka hatua ya awali ya michuano ya ligi ya mabingwa, 'focus' ya Wananchi sasa imerudi kwenye ligi.
Wakiwa kileleni mwa msimamo wa ligi, Wananchi watashuka KMC Complex kuzisaka alama tatu muhimu ambazo zitawahakikishia kuendelea kusalia kileleni kabla kukutana na watani zao Simba kwenye mchezo unaofuata baada ya mapumziko ya kalenda ya FIFA.
Akizungumza na wanahabari jana, Kocha Mkuu wa Yanga Manqoba Mngqithi aliweka bayana kuwa Geita Gold sio timu nyepesi na anatarajia kukutana na upinzani mkali.
Hata hivyo Mngqithi alisisitiza kuwa kikosi chake kiko tayari kwa ushindani wa aina yoyote wakihitaji kushinda na kusalia katika nafasi yao.
Yanga imeanza msimu huu kibabe ikiwa na rekodi ya ushindi kwa asilimia 100 baada ya kushinda mechi zote za tano za kwanza.
Leo watakuwa na nafasi ya kuendeleza rekodi hiyo kwenye uwanja wa nyumbani.
