Baada ya kukosekana uwanjani kwa takribani msimu mzima, habari njema kwa mashabiki wa Yanga ni kurejea kikosini kwa mshambuliaji Clement Mzize.
Yanga imethibitisha kuwa Mzize leo atakuwa sehemu ya wachezaji ambao wataikabili Geita Gold katika mchezo wa ligi kuu ya NBC.
Ni rasmi Bull Striker Mzize anarejea tena kuwapa burudani Wananchii..!
