Jana Yanga ilifanikiwa kuendeleza kasi yake kwenye ligi kuu msimu huu wakiichapa Geita Gold bao 1-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa KMC Complex.
Katika mchezo huo mashabiki wa Yanga walimshuhudia mshambuliaj Clement Mzize akirejea kikosini baada ya kuwa nje ya uwanja kwa takribani miezi 7.
Akizungumza baada ya mchezo, Kocha Mkuu wa Yanga Manqoba Mngqithi alieleza kufurahishwa na kiwango kilichoonyeshwa na mshambuliaji huyo akibainisha wazi kuwa Mzize ni mmoja wa wachezaji wake muhimu msimu huu.
Manqoba amesema kama mshambuliaji huyo atakuwa fit haraka ni wazi atakuwa msaada mkubwa kwa Yanga msimu huu.
"Mzize amecheza vizuri sana, licha ya kuwa amerejea baada ya kukaa nje kwa takribani miezi saba. Nii miongoni mwa wachezaji muhimu katika mipango yetu msimu huu, natamani aendelee kuwa fiti," alisema Manqoba.


Mngqithi pia alibainisha kuwa beki Dickson Job nae anakaribia kurejea uwanjani huku akisisitiza umuhimu wa kuwa na kikosi kamili na wachezaji wote wakiwa katika hali nzuri ya utimamu wa mwili.
Katika hatua nyingine Manqoba ametetea uamuzi wake wa kufanya 'rotation' ya kikosi akisisitiza umuhimu wa kuwapa mapumziko wachezaji waliotumika zaidi ili kuwaepusha na changamoto za majeraha.
Katika mchezo huo Mngqithi hakuwatumia kabisa Yao Kouassi, Chadrack Boka, Bakari Mwamnyeto, Albert Kangwanda na Peter Shalulile ambaye ilielezwa alipata majeraha ya nyonga kwenye mchezo uliopita wa ligi ya mabingwa.