Kampuni ya SportPesa ambao ni Wadhamini wakuu wa klabu ya Yanga 2022-25, imeeleza kusikitishwa na hatua ya Yanga kuitangaza kampuni ya Haier kuwa Mdhamini katika michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika
Taarifa iliyotolewa na SportPesa mapema leo, imebainisha kuwa kampuni hiyo ilipendekeza Yanga kutumia 'Visit Tanzania' kama mbadala katika michuano hiyo
Hata hivyo Yanga haikukubaliana na mapendekezo hayo na kuamua kusaini mkataba maalum na Haier kuwa wadhamini katika michuano ya Shirikisho tu
SportPesa wametaka fidia kutoka kwa klabu ya Yanga




