Ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Alliance Girls leo umeifanya Simba Queens izidi kusogea juu kwenye msimamo wa ligi kuu ya Wanawake 'Serengeti Lite'
Simba Queens iko nyuma ya vinara wa ligi hiyo JKT Queens kwa tofauti ya alama moja baada ya kufikisha alama 16
JKT Queens leo wamelazimishwa suluhu ya bila kufungana dhidi ya Yanga Princess na kufikisha alama 17

Fountain Gate nao wamelazimishwa suluhu ya bila kufungana dhidi ya Ceasiaa Queens hivyo kufikisha alama 16 lakini wameshuka nafasi ya tatu kwa tofauti ya mabao dhidi ya Simba Queens
Mwanadada Jentrix Shikangwa alikuwa shujaa wa Simba Queens leo akifunga mabao yote