Ruvu Shooting yahamia Morogoro

Joel JJ By Joel JJ β€’ 2nd February 2023


Ruvu Shooting yahamia Morogoro

Baada ya kufanya vibaya katika mechi zake mbalimbali walizocheza kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam kama uwanja wake wa nyumbani, Ruvu Shooting imetangaza kuhamia kwenye Uwanja wa Jamhuri mkoani, Morogoro

Ofisa Habari wa Ruvu Shooting, Masau Bwire, alisema mechi yao ya kwanza kutumia Uwanja wa Jamhuri itakuwa dhidi ya KMC FC ya Dar es Salaam ambayo itachezwa Jumapili.

"Tayari taratibu zote zimeshakamilika, Jumapili tutaanza kuutumia rasmi Uwanja wa Jamhuri, Morogoro kama uwanja wetu wa nyumbani, nadhani baada ya hapo tutakuwa na mwendelezo mzuri kwa sababu kule ni kama nyumbani tu Pwani," alisema Bwire.

Hata hivyo, Bwire alikwepa kuhusisha uamuzi wa kuhama uwanja umetokana na matokeo mabaya waliyopata wakati wakicheza kwenye Uwanja wa Uhuru baada ya Uwanja wao wa Mabatini ulioko Mlandizi, Pwani kufungiwa.

"Uwanja hauchezi, unaocheza ni mpira, kama uwezo mdogo hata wakupeleke chumbani mwako watu watakufunga tu. Sisi tumejidhatiti kwenye uwezo na wala si kwa sababu tunapoteza sana Uhuru, ila Uwanja wa Jamhuri tuliuchagua tangu awali wakati uwanja wetu wa Mabatini Mlandizi ulipofungiwa," aliongeza ofisa huyo.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.