Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi, Februari 02 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 2nd February 2023


Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi, Februari 02 2023

Everton wanataka kumsajili mshambuliaji wa Ghana Andre Ayew, ambaye anatarajiwa kuwasili Uingereza kwa mazungumzo, kwa uhamisho wa bure. Nottingham Forest pia inaweza kujaribu kumnunua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33. (Mail)

The Toffees pia wanaweza kutafuta kumsajili kiungo wa kati wa zamani wa Real Madrid na Uhispania Isco, 30, ambaye anapatikana kwa uhamisho wa bure. (Times - usajili unahitajika)

Everton ilishindwa kumnunua mshambuliaji wa Colombia Duvan Zapata mwenye umri wa miaka 31 baada ya ombi lao kukataliwa na Atalanta. (TeamTalk)

Hilo lilikuwa moja ya malengo 14 yaliyoripotiwa ambayo Everton ilishindwa kusaini siku ya mwisho. (Express)

Beki wa Chelsea na England Ben Chilwell, 26, ni miongoni mwa wachezaji wanaolengwa na Manchester City msimu huu wa joto ikiwa mlinzi wa Ureno Joao Cancelo, 28, hatarejea kutoka kwa muda wake wa mkopo Bayern Munich. (Times - usajili unahitajika)

Wamiliki wa Chelsea hawatadai matokeo ya haraka kutoka kwa meneja Graham Potter kufuatia matumizi mabaya ya fedha ya mwezi Januari. (Guardian)

The Blues wanatazamiwa kuongeza usajili mwingine katika mshambuliaji Muingereza Jimmy-Jay Morgan, 17, ambaye atajiunga nao kutoka Southampton. (Sun)

Winga wa Chelsea kutoka Morocco Hakim Ziyech, 29, alituma ujumbe mfupi wa maandishi kwa mmiliki wa klabu Todd Boehly alipokuwa akijaribu kukamilisha uhamisho wake wa mkopo kwenda Paris St-Germain. (Mirror)

Leeds United ilikataa nafasi ya kumsajili beki Mwingereza Axel Tuanzebe, 25, kwa mkopo kutoka Manchester United kabla ya dirisha la Januari kufungwa. (The Athletic, kupitia Metro)

Wakala wa mshambuliaji wa Liverpool na Brazil Roberto Firmino, 31, anaamini kuwa mazungumzo kuhusu kandarasi mpya katika klabu hiyo yatakamilika mwezi huu. (Sky Germany, kupitia Mirror)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.