Kocha Msaizidi wa Yanga Cedric Kaze amesema wamekamilisha maandalizi kuelekea mchezo wa ligi kuu dhidi ya Namungo Fc ambao utapigwa kesho Jumamosi katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Kaze amesema wamejiandaa kukabiliana na mechi ngumu dhidi ya Namungo ambao wana kikosi imara kilichoongezewa ubora katika usajili wa dirisha dogo
"Mechi dhidi ya Namungo Fc haijawahi kuwa rahisi, tunafahamu ni moja ya timu zinazocheza soka la ushindani kwenye ligi. Tunacheza katika uwanja wetu wa nyumbani, najua tutakuwa na sapoti kubwa kutoka kwa mashabiki wetu hivyo tutahakikisha tunapata matokeo mazuri," alisema Kaze
Kaze aliongeza kuwa wachezaji wawili watakosekana katika mchezo huo wakiwa ni majeruhi
"Golikipa Aboutwalib Mshery bado ni majeruhi wakati Denis Nkane ndio ameanza mazoezi mapesi akitoka kwenye majeraha. Wachezaji wengine tunawaangalia baada ya mazoezi ya mwisho leo tutajua kama tutawatumia au la"
"Lakini naweza kuhakikisha kuwa Khalid Aucho atatumika siku ya kesho," alisema Kaze