Ruvu Shooting yazinduka, yaichapa KMC 2-1

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th February 2023


Ruvu Shooting yazinduka, yaichapa KMC 2-1

Wakicheza mechi yao ya kwanza kwenye uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro, Ruvu Shooting leo wamepata ushindi wao wa kwanza kwenye ligi baada ya muda mrefu wakiifunga KMC mabao 2-1

Ni ushindi wa nne kwa Ruvu Shooting msimu huu, ushindi ambao unaweza kuwaongezea matumaini katika vita ya kuwania kubaki ligi kuu

Ushindi huo umewafanya wasogee mpaka nafasi ya 15 kwenye msimamo wa ligi wakiishusha chini Polisi Tanzania ambayo inasubiri kucheza na Kagera Sugar

Aidha mechi iliyopigwa mapema, Ihefu Fc waliibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Mbeya City

Ihefu Fc 'gari limewaka' kwani wameshinda mechi nne kati ya tano zilizopita


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.