Wakicheza mechi yao ya kwanza kwenye uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro, Ruvu Shooting leo wamepata ushindi wao wa kwanza kwenye ligi baada ya muda mrefu wakiifunga KMC mabao 2-1
Ni ushindi wa nne kwa Ruvu Shooting msimu huu, ushindi ambao unaweza kuwaongezea matumaini katika vita ya kuwania kubaki ligi kuu
Ushindi huo umewafanya wasogee mpaka nafasi ya 15 kwenye msimamo wa ligi wakiishusha chini Polisi Tanzania ambayo inasubiri kucheza na Kagera Sugar
Aidha mechi iliyopigwa mapema, Ihefu Fc waliibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Mbeya City
Ihefu Fc 'gari limewaka' kwani wameshinda mechi nne kati ya tano zilizopita



