Ushindi wa mabao 3-0 ambao Fc Barcelona waliupata dhidi ya Sevilla hapo jana, umewafanya waendelee kujichimbia kileleni mwa La Liga sasa kwa tofauti ya alama nane
Real Madrid walikumbana na kipigo kisichotarajiwa kutoka kwa Mallorca wakichapwa bao 1-0 katika mchezo uliopigwa mapema hapo jana
Jordi Alba, Gavi na Rafihna ndio walioihakikishia Barcelona ushindi huo katika mchezo uliopigwa saa 5 usiku
Fc Bercelona wamekuwa na kiwango bora msimu huu, wanajiweka katika nafasi nzuri ya kutwaa taji la La Liga
Wamekusanya alama 53 kutoka mechi 20 wakifuatiwa na Real Madrid yenye alama 45 kutoka mechi 20 pia



