Bao alilofunga katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Manchester City hapo jana limemfanya Harry Kane kuwa mfungaji bora wa muda wote wa klabu ya Tottenham Hotspurs akifikisha mabao 267
Kane amevunja rekodi ya mabao 266 iliyowekwa na Jimmy Greaves ambayo ilidumu kwa ziadi ya miaka 50
Aidha Kane pia ameingia kwenye historia ya wachezaji waliofunga mabao 200 au zaidi katika ligi kuu ya Uingereza
Yuko nyuma ya Alan Shearer aliyefunga mabao 260 na Wayne Rooney aliyefunga mabao 208
Katika msimu huu Kane amefunga mabao 17 kwenye ligi kuu ya Uingereza akiwa nyuma kwa tofauti ya mabao nane dhidi ya Haaland wa Manchester City aliyefunga mabao 25



