KMC hali ni tete Ligi kuu

Joel JJ By Joel JJ β€’ 7th February 2023


KMC hali ni tete Ligi kuu

Watoza ushuru wa Manispaa ya Kinondoni, KMC wanakabiliwa na ukata wa ushindi katika ligi kuu ya NBC

Katika michezo 14 ya Ligi Kuu iliyopita KMC imeshinda mechi mbili tu. Ni matokeo mabaya zaidi kwa timu hiyo na sasa ligi ikiwa inaelekea ukingoni

Kwenye mechi hizo 14 zilizopita, KMC ilipata ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Coastal Union na ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Polisi Tanzania.

Mechi nyingine 12 wamepata sare 4 na kupoteza mechi nane (8). Kwenye mechi tano (5) zilizopita, KMC imepoteza mechi nne (4) na kuambulia sare moja (1).

Kwa maana hiyo, katika mechi tano (5) zilizopita KMC imepata alama moja tu

Wapo nafasi ya 12 kwenye msimamo wa Ligi wakiwa na alama 23 tofauti ya alama moja (1) na Tanzania Prisons ambao wapo nafasi ya 13 wakiwa ni sehemu ya kucheza play offs kubaki Ligi Kuu.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.