Yanga

Yanga kuifuata US Monastir leo

King kong By King kong
β€’
7 Feb 2023
Yanga kuifuata US Monastir leo

Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amesema kikosi cha Yanga kinaondoka leo jijini Dar es salaam majira ya saa 9 kuelekea Tunisia kupitia Dubai ambako watawasili majira ya saa ya 3:50 usiku

Kesho asubuhi saa 2:40 Yanga itaondoka Dubai kuelekea Tunis tayari kwa mchezo dhidi ya Monastir

Mchezo utapigwa katika dimba la Stade Olympique Hammadi Agrebi Jumapili Februari 12 kwa kuwa uwanja wa Monastir haukukidhi vigezo vya CAF

Uwanja wa Olympique Hammadi Agrebi ndipo Yanga ilishinda dhidi ya Club Africain

Yanga inaondoka na wachezaji 25 akiwemo mlinda lango Aboutwalib Mshery ambaye anakwenda Tunisia kwa ajili ya matibabu

Viongozi tisa wako kwenye msafara huo ambapo Mkuu wa msafara ni Seif Gulamali kwa upande wa Yanga

Kocha Nasreddine Nabi tayari ametangulia Tunisia

Katika hatua nyingine, Kamwe ametangaza viingilio kuelekea mchezo wao wa kwanza wa nyumbani dhidi ya TP Mazembe ambao utapigwa Februari 19 kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa

Kamwe amesema dhamira yao ni kuona wanaujaza uwanja wa Benjamin Mkapa na kuhakikisha wanashinda mchezo huo na nyingine mbili zitazofuata ili kufikia malengo ya kutinga robo fainali

"Historia inaonyesha hatukuwa na matokeo mazuri kwenye hatua ya makundi katika miaka ya nyuma lakini msimu huu tuko tayari, tumedhamiria kufanya vizuri na kutinga robo fainali"

"Tunataka mashabiki wetu wawe na utamaduni wa kununua tiketi mapema ndio maana tumetangaza bei za vingilio vya mchezo wetu wa kwanza nyumbani dhidi ya TP Mazembe ambao utapigwa Jumapili, Februari 19"

"VIP A ni Tsh 30,000/-, VIP B ni Tsh 20,000/-, VIP C ni Tsh 10,000/- na Mzunguuko ni Tsh 3,000/- kama utanunua tiketi yako sasa na Tsh 5,000/- kama utanunua tiketi siku ya mchezo"

"Tunajua umuhimu wa alama tisa katika mechi za nyumbani hivyo tunaanza na TP Mazembe, ni lazima tuhakikishe alama zote tatu zinabaki," alisema Kamwe

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
5h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
5h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
5h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
9h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
12h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
13h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
14h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
14h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
15h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
16h ago
READ MORE β†’