Yanga

Yanga yatua Tunisia, madaktari wake waokoa mgonjwa kwenye ndege

Joel JJ By Joel JJ
β€’
8 Feb 2023
Yanga yatua Tunisia, madaktari wake waokoa mgonjwa kwenye ndege

Madaktari wa Yanga wameokoa uhai wa abiria mmoja wakati kikosi hicho kikiwa safarini kwenda nchini Tunisia kwa ajili ya mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya US Monastir utakaochezwa Jumapili ya Februari, 12

Kwa mujibu wa kituo cha redio cha UFM wakati timu hiyo ikiwa safarini rubani wa ndege la Shirika la Emirates alisikika kupitia vipaza sauti akisema;

"Tunaomba kama kuna daktari yoyote apite mbele, tuna mgonjwa yupo kwenye hali ya hatari."

Jitihada za madaktari wa Yanga za kuokoa maisha ya abiria huyo zilizaa matunda baada ya kupatiwa matibabu na kurejea kwenye hali yake ya kawaida jambo ambalo liliifanya ndege hiyo kuendelea na safari na kutua jiji la Tunis kwa wakati uliotakiwa.

Kwa mujibu wa Daktari wa Yanga, Moses Etutu alinukuliwa akisema abiria huyo alikuwa na changamoto ya sukari pamoja na mambo mengine.

Aidha kwa taarifa iliyotolewa na wahudumu wa ndege ilikuwa inahitaji kutua uwanja wa karibu ili kuokoa maisha ya abiria huyo ingawa jitihada za madaktari wa Yanga ziliwafanya kusitisha mpango huo na kuendelea na safari kama ilivyopangwa.

More Stories

Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
2h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
6h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
6h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
7h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
8h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
8h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
9h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
10h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
23h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
23h ago
READ MORE β†’