Simba

Tumeisoma Horoya Ac - Mgunda

Joel JJ By Joel JJ
β€’
8 Feb 2023
Tumeisoma Horoya Ac - Mgunda

Kocha Msaidizi wa Simba, Juma Mgunda, amesema tayari wamefanikiwa kuona ubora wa Horoya AC ulipo na udhaifu wao, hivyo wataenda nchini Guinea kikamilifu kwa ajili ya kusaka pointi muhimu katika mchezo huo wa hatua ya makundi wa Ligi ya Mabingwa Afrika

Simba inatarajiwa kuondoka nchini Alfajiri ya Alhamisi kuelekea Guinea tayari kwa mchezo huo utakaopigwa Jumamosi, Februari 11

Mgunda amesema wanafahamu wanaenda kucheza na aina gani ya timu na wamejiandaa vizuri kwa ajili ya kusaka matokeo chanya.

Amesema wanahitaji kupata matokeo mazuri, hivyo wamewaelekeza wachezaji wao kuwa makini kwa kutumia vizuri nafasi wanazotengeneza kupata bao na kutoruhusu Horoya AC kufanya mashambulizi lango mwao.

"Tumeona ubora wa Horoya AC, wako vizuri, tunaenda kwa tahadhari kubwa, wachezaji wanatambua umuhimu wa mchezo huo ni kutafuta pointi, tunaendelea kuimarisha kikosi hususan safu ya ulinzi kuwa makini na washambuliaji wa timu pinzani"

"Wakati tukipambana wapinzani wasipate bao, tunahitaji kuwa makini kutafuta alama hata moja katika mchezo huo wa ugenini kabla ya kurejea nyumbani kwa ajili ya kutafuta pointi tatu za nyumbani," alisema Mgunda

More Stories

Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
1h ago
READ MORE β†’
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
11h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
11h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
12h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
15h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
19h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
19h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
20h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
20h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
21h ago
READ MORE β†’