Liverpool ni miongoni mwa vilabu vinavyovutiwa na mlinzi wa Everton Jarrad Branthwaite, 20, ambaye yuko kwa mkopo PSV Eindhoven. Manchester United na Roma pia wanamfuatilia beki huyo wa kati wa England chini ya miaka 20. (Mail)
Mshambuliaji wa Gabon Pierre-Emerick Aubameyang, 33, yuko mbioni kuondoka Chelsea na kwenda Los Angeles FC.(Le10 Sport, via Metro).
Chelsea wapo kwenye mazungumzo ya mwisho mwisho na Thiago Silva kuhusu mkataba mpya wa mlinzi huyo wa Brazil utakaomvusha zaidi ya miaka 39 ya kuzaliwa kwake mwezi Septemba. (London Evening Standard)
Arsenal, Liverpool na Newcastle zote zinavutiwa na kiungo wa kati wa Ajax na Mexico Edson Alvarez, 25. (Caught Offside)
Arsenal pia wanaweza kuimgia katika mbio za kutaka kumnunua kiungo wa kati wa Real Sociedad Mhispania Martin Zubimendi, 24, msimu huu kutokana na Barcelona kuelekeza nguvu zao za uhamisho kwingine. (Mirror)
Everton itafanya jaribio lingine la kumnunua mshambuliaji wa Ureno Beto, 25, kutoka Udinese ya Italia msimu wa joto baada ya kushindwa kufikia makubaliano mwezi Januari. (Mondo Udinese)
Leeds United imekataliwa na kocha wa Rayo Vallecano Mhispania Andoni Iraola, 40, kuchukua nafasi ya mkufunzi aliyetimuliwa Jesse Marsch huku timu hiyo ya Ligi kuu ikikabiliwa na hali ngumu zaidi katika kujaribu kumteua meneja mpya. (Onda Cero, via Express)
Tottenham inaweza kumsajili mlinda mlango wa zamani wa Manchester United na England Ben Foster, 39 kama mbadala wa Hugo Lloris, ambaye atakuwa nje kwa angalau wiki sita kutokana na jeraha la goti. Foster alitangaza kustaafu Septemba mwaka jana lakini anaweza kujiunga kwa mkopo wa muda mfupi. (Mirror)
Manchester United wametiwa moyo katika harakati zao za kumnunua kiungo wa kati wa Barcelona na Uholanzi Frenkie de Jong, 25, na mshambuliaji wa Uhispania Ansu Fati, 20, kutokana na La Liga kuwataka wababe hao wa Catalan kupunguza bili yao kubwa ya mishahara. (Mundo Deportivo, via Mail)
Mshambuliaji wa zamani wa Arsenal Olivier Giroud anatarajiwa kujadili mkataba mpya na AC Milan. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa, 36, alikuwa akisakwa na Everton mwezi Januari. (Fabrizio Romano) Mshambuliaji Joao Mendes, 17, mtoto wa gwiji wa Brazil Ronaldinho, anakaribia kujiunga na Barcelona baada ya kufuzu majaribio Nou Camp. (Star)
Kiungo nyota wa Kombe la Dunia wa Morocco Sofyan Amrabat, 26, alijitolea kucheza bila malipo ili kupata uhamisho wa kwenda Barcelona kutoka Fiorentina. (Mundo Deportivo, via Sun)
BBC