Mabao ya Marcus Rashford na Jadon Sancho yaliinusuru Manchester United na kupigo kutoka kwa Leeds United katika mchezo Ligi Kuu ya Uingereza uliopigwa dimba la Old Trafford
Gnonto aliitanguliza Leeds kwa bao la mapema dakika ya kwanza kabla ya Verane kujifunga bao la pili kuipa Leeds uongozi usiotarajiwa wa mabao 2-0
Ikumbukwe Leeds waliingia kwenye mchezo huo wakiwa hawana kocha baada ya kumtimua Jesse Marsch siku ya Jumatatu
Ni matokeo ambayo yanazidi kuvuruga hesabu za United katika mbio za ubingwa kwani sasa wako nyuma ya vinara Arsenal kwa tofauti ya alama 7
Arsenal wana mechi mbili za viporo



