Halmashauri ya mji wa Geita imeweka wazi kuwa inatazamia kufanyia mabadiliko uwanja wake mpya na kuondoa nyasi za asili zilizopandwa, ili kuweka nyasi bandia.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Geita, Costantine Moradi ametoa taarifa hiyo katika mkutano Mkuu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Geita (GEREFA).
Morandi amesema hadi sasa ujenzi wa uwanja unaendelea na nyasi za asili zilishapandwa, lakini ukaguzi wa mhandisi mshauri umebaini kuna mabonde chini ya nyasi.
"Kwa hiyo tumekubaliana hivyo, yule mtaalamu wa TFF (Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania) aliyekuja, tumempa maelekezo atueleze gharama za kuweka nyasi bandia, tena zile za kiwango cha juu.
"Alitueleza kuna nyasi za viwango vitatu, kwa maana ya A, B na C, na sisi tumemwambia tunataka zile nyasi zenye ubora wa daraja A kama zilizopo chamazi," alisema Moradi



