Simba - Horoya Ac

Simba tayari kuzisaka alama tatu Guinea

Joel JJ By Joel JJ
β€’
10 Feb 2023
Simba tayari kuzisaka alama tatu Guinea

Leo majira ya saa 1 usiku Simba itakamilisha maandalizi kuelekea mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika

Mchezo huo utafanyika katika uwanja wa Septemba 28, saa 1 usiku. Simba itafanya mazoezi ya mwisho katika uwanja huo

Habari njema kwa Simba ni kuwa mchezo huo utachezwa bila ya mashabiki na pengine ndio mchezo pekee ambao Horoya watacheza huko Guinea

Uwanja wa Septemba 28 umekosa sifa kulingana na vigezo vya CAF, Horoya wameruhusiwa kuutumia kwa mchezo dhidi ya Simba tu na katika nchi ya Guinea hakuna uwanja mwingine ulioidhinishwa na CAF

Horoya Ac watalazimika kwenda kucheza mechi zao ya nyumbani kwenye nchi jirani

Simba imekuwa gumzo katika Mji wa Konakr, mashabiki wengi wa soka nchini Guinea wanaifahamu Simba kutokana na mafanikio yake kwenye michuano ya ligi ya mabingwa

Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amesema wametua Guinea wakiwa na dhamira moja, kusaka ushindi na kama watakosa basi wataridhika kurudi na alama moja nyumbani

Simba iko kundi C pamoja na Horoya Ac, Raja Casablanca na Vipers

Raja Casablanca itachuana na Vipers Fc leo katika utakaopigwa saa 4 usiku

More Stories

Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
33m ago
READ MORE β†’
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
10h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
11h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
11h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
14h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
18h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
18h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
19h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
20h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
20h ago
READ MORE β†’