Vipers Fc wamekaribishwa hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika kwa kipigo cha mabao 5-0 kutoka kwa Raja Casablanca
Mabingwa hao wa Uganda ni mara yao ya kwanza kushiriki hatua ya makundi ya michuano hiyo
Leo mchezo mwingine wa kundi C kati ya Horoya AC dhidi ya Simba utapigwa huko Guinea
Mechi muhimu kwa Simba kuanza vyema michuano hiyo katika mkakati wao wa kucheza nusu fainali
Mechi nyingine iliyopigwa jana, iliwashuhudia mabingwa wa Misri Zamalek wakiwa nyumbani, wakikubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa CR Belouizdad
Mechi nyingine za michuano hiyo zinaigwa leo, Mamelod Sundowns wakichuana na Al Hilal katika moja ya mechi hizo
Al Hilal waliweka kambi ya siku 10 nchini kujiandaa na mchezo huo utakaopigwa saa 10 jioni



