Vipers hoi, Horoya Ac vs Simba ni leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 11th February 2023


Vipers hoi, Horoya Ac vs Simba ni leo

Vipers Fc wamekaribishwa hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika kwa kipigo cha mabao 5-0 kutoka kwa Raja Casablanca

Mabingwa hao wa Uganda ni mara yao ya kwanza kushiriki hatua ya makundi ya michuano hiyo

Leo mchezo mwingine wa kundi C kati ya Horoya AC dhidi ya Simba utapigwa huko Guinea

Mechi muhimu kwa Simba kuanza vyema michuano hiyo katika mkakati wao wa kucheza nusu fainali

Mechi nyingine iliyopigwa jana, iliwashuhudia mabingwa wa Misri Zamalek wakiwa nyumbani, wakikubali kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa CR Belouizdad

Mechi nyingine za michuano hiyo zinaigwa leo, Mamelod Sundowns wakichuana na Al Hilal katika moja ya mechi hizo

Al Hilal waliweka kambi ya siku 10 nchini kujiandaa na mchezo huo utakaopigwa saa 10 jioni


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.