Transfer

Tetesi za soka barani Ulaya, Jumapili Februari 12 2023

Joel JJ By Joel JJ
12 Feb 2023
Tetesi za soka barani Ulaya, Jumapili Februari 12 2023

Klabu ya Liverpool huenda ikakubali kuwauza wachezaji wake nyota mwishoni mwa msimu ikiwemo mshambuliaji kinara kutoka Misri Mohamed Salah, 30. (Football Insider)]

Real Madrid wamefanya mawasiliano na kocha wa Liverpool Mjerumani Jurgen Klopp, 55, juu ya uwezekano wa kuchukua mikoba ya Mtaliano Carlo Ancelotti, 63, ya kuinoa miamba hiyo ya Uhispania kuanzia msimu ujao. (El Nacional - in Catalan)

Liverpool watakubali ofa ya wastani wa pauni milioni 15 ili kumuuza beki wa raia wa Cameroon, Joel Matip. (Football Insider)

Baadhi ya maafisa wa Chelsea wamechoshwa na hatua ya kiungo wao raia wa England Mason Mount, 24, kukataa kusaini mkataba mpya na klabu hiyo. (Telegraph)

Manchester United wapo katika mazungumzo na mshambuliaji wao kinara raia wa England Marcus Rashford, 25, ili aongeze mkataba. (GiveMeSport)

Newcastle wanasuka mpango wa kumsajili kiungo wa klabu ya Lazio na timu ya taifa ya Serbia Sergej Milinkovic-Savic, 27, ambaye ana mkataba na klabu yake mpaka mwaka 2024. (Il Messagero, via Goal)

Manchester United wana nia ya kumsajili mshambuliaji wa klabu ya Roma na raia wa Argentina Paulo Dybala, 29. (Calciomercato - in Italian)

Mshambuliaji wa Atletico Madrid na timu ya taifa ya Ureno Joao Felix, 23, ambaye kwa sasa yupo Chelsea kwa mkopo, ndiye mchezaji kinara atakayewindwa na Real Madrid katika dirisha la usajili la mwishoni mwa msimu katika majira ya kiangazi.(Fichajes - in Spanish)

Paris St-Germain wanahaha kumnyakua kocha wa Manchester City Mhispania Pep Guardiola, 52. (El Nacional - in Catalan)

Nahodha na mshambuliaji kinara wa timu ya taifa ya England na klabu ya Tottenham Hotspur Harry Kane, 29, anatazamiwa kukataa ofa ya kujiunga na timu yoyote kubwa barani Ulaya ili kusalia katika Ligi ya Primia mwishoni mwa msimu huu. (Football Insider)

Kiungo wa klabu ya Barcelona na raia wa Ivory Coast Franck Kessie, 26, alikataa kujiunga na klabu ya Tottenham Hotspur katika dirisha dogo l usajili la mwezi Januari. (Sport - in Spanish)

Wapinzani wa jadi klabu za AC Milan na Inter Milan wote wanamtazamia kocha wa sasa wa klabu ya Lazio Maurizio Sarri, 64, kuwa kocha Mkuu wa klabu zao katika siku za usoni. (Il Messaggero, via Football Italia)

Nahodha na kiungo nyota wa zamani wa Liverpool Steven Gerrard, 42, is "ana nia ya hali ya juu" ya kuchukua usukani wa kuinoa klabu ya Leeds ambayo hivi karibuni walimtimua kocha kutoka Marekani Jesse Marsch. (Football Insider)

BBC

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
7h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
8h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
10h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
10h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
11h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
11h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
12h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
12h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
12h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
14h ago
READ MORE →