Mchezo wa kwanza kwa Yanga hatua ya makundi kombe la Shirikisho umemalizika kwa Wananchi kukubali kipigo cha mabao 2-0 dhidi ya US Monastir huko Tunisia
Monastir walifunga mabao yao kwenye dakika 16 za kwanza kupitia mipira ya kichwa kutoka kwa Muhamed Sakhroul na Bobacar Traore wakitumia makosa ya safu ya ulinzi ya Yanga katika kucheza mipira ya krosi
Ni mabao yaliyofanana na aina ya mabao ambayo Yanga imekuwa ikiruhusu kupitia mipira hiyo
Yanga ilitawala mchezo huo kwa muda mwingi kitu pekee ambacho kitawasononesha Wananchi ni timu yao kutofunga walau bao moja
Mchezo unaofuata ni dhidi ya TP Mazembe, utapigwa Jumapili ijayo katika uwanja wa Benjamin Mkapa