Tetesi za soka Jumatatu, Februari 13 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 13th February 2023


Tetesi za soka Jumatatu, Februari 13 2023

Liverpool wameingia kwenye kinyang'anyiro cha kuwania saini ya Victor Osimhen kutoka Napoli. Mshambuliaji huyo wa Nigeria mwenye umri wa miaka 24 pia anasakwa na Manchester United. (Fichajes - kwa Kihispania)

Chelsea ni miongoni mwa vilabu vinavyomfuatilia mlinda mlango wa Brentford na Uhispania David Raya, 27. (Football.London)

Chelsea pia wanataka kumsajili winga wa Barcelona na Morocco Abde Ezzalzouli. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 kwa sasa yuko kwa mkopo Osasuna. (Mundo Deportivo - kwa Kihispania)

Liverpool wanataka kumsajili mlinda mlango wa Anderlecht Mholanzi Bart Verbruggen kwa nia ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20 kuwa mlinda mlango wao nambari moja. (Sun)

Mkufunzi mpya wa Everton Sean Dyche amepatia umuhimu mkubwa mlinda mpango wa mlango wa Uingereza Jordan Pickford, 28, kusaini mkataba mpya katika klabu hiyo. (Sun)

Kocha zamani wa Leeds Jesse Marsch huenda akaajiriwa Southampton baada ya kuondoka kwa Nathan Jones Jumapili, wiki moja baada ya kuondoka Elland Road. (Athletic- Usajili unahitajika)

Southampton pia wanavutiwa na kocha wa Torino Ivan Juric. (Mail)

Newcastle wako mbele ya Liverpool na Barcelona katika mbio za kuwania saini ya kiungo wa kati wa Eintracht Frankfurt na Japan Daichi Kamada, 26. (CaughtOffside).

Klabu za Southampton na Leeds zinamtaka kocha wa Argentina Marcelo Gallardo, 47, kuwa meneja wao mpya. (Football Insider)

Mshambuliaji wa Flamengo na Brazil Pedro, 25, yuko kwenye rada za West Ham. (Fichajes - kwa Kihispania)

Crystal Palace inamfuatilia mshambuliaji wa Celtic na Japan Kyogo Furuhashi, 28. (Football Insider)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.