Nyota wa Argentina na mshindi wa kombe la Dunia 2022 Lionel Messi ameripotiwa kutaka kuondoka Paris Saint German licha ya ripoti za hivi kribuni kuashiria kuwa na uwezekano wa kusaini mkataba mpya wa kuendelea kuitumikia miamba hiyo ya Ufaransa.
Japo mpango wa kuongeza mkataba wa mwaka mmoja wa kusalia Jijini Paris bado ni chaguo kwa Messi lakini, haionekani kuwa kipaumbele cha nyota huyo wa zamani wa Barcelona kwa sasa.
Vilabu vya Barcelona na Inter Miami vimeonesha nia ya kutaka saini ya mshindi huyo mara 7 wa Ballon d'or
Inaelezwa kuwa Messi anasita kuhamia MLS, ikizingatiwa kwamba anataka kusalia kuwa sehemu ya timu ya taifa ya Argentina kuelekea Copa America 2024
Messi (35) umeonekana kuimarika kwa kiwango kikubwa msimu huu ikilinganishwa na mwaka wake wa kwanza huko Paris
Msimu huu Messi amefunga mabao 15 katika michuano yote



