Kikosi cha Yanga SC kimetua jijini Dar leo kikitoka Tunisia ambapo walicheza mechi ya kwanza ya makundi Kombe la Shirikisho dhidi ya US Monastir na kufungwa mabao 2-0
Mechi ijayo Yanga itakuwa mwenyeji kwenye uwanja wa Mkapa dhidi ya TP Mazembe Jumapili Februari 19 saa 1:00 usiku
Akizungumza baada ya kuwasili, Kocha Mkuu wa Yanga Nasreddine Nabi alisema hawakufurahishwa na matokeo ya kufungwa na US Monastir katika mchezo ambao hawakustahili kipigo
Nabi alisema walifungwa mabao mepesi ambayo hawapaswi kufungwa katika ngazi hii ya mashindano
"Tuna masikitiko kwa sababu tulichokipata hatukustahili. Tumefungwa mabao mawili kupitia mipira ya kutenga, hatupaswi kufungwa mabao ya aina hiyo katika ngazi hii"
"Tumeumia na tunajua mashabiki wetu nao wameumia. Hilo linatufanya tujipange sawa sawa ili kuhakikisha tunashinda mchezo unaofuata," alisema Nabi



