Arsenal - Manchester City

Arsenal hoi mbele ya Manchester City

Joel JJ By Joel JJ
β€’
16 Feb 2023
Arsenal hoi mbele ya Manchester City

Wakiwa katika uwanja wao wa Emirates, Arsenal wameshindwa kutamba mbele ya Manchester City wakikubali kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa mabingwa hao watetezi wa Ligi ya Premia

Ni matokeo ambayo sio tu kuwa yanawatia hofu mashabiki wa Arsenal waliojaa matumaini kuwa msimu huu wanaweza kuwa mabingwa baada ya kusubiri kwa miaka 19, bali pia yamewaonyesha Mikel Arteta ana kazi ya kufanya ili kutimiza ndoto hiyo

Ulikuwa mchezo ambao Arsenal walitawala kwa muda mwingi lakini City wakatumia nafasi muhimu walizopata kupata ushindi

Kelvin De Bruyne alitumia makosa ya mlinzi Takehiro Tomiyasu kurudisha mpira mfupi kwa kipa kuiandikia City bao la kuongoza kwenye dakika ya 24

Arsenal wakakomboa bao hilo kupitia mkwaju wa penati kwenye dakika ya 42 baada ya Nketiah kufanyiwa madhambi na mlinda lango wa City Ederson

Manchester City walikuwa bora zaidi kwenye kipindi cha pili na kufanikiwa kuongeza mabao mengine mawili kupitia kwa Glealish na Haaland aliyefunga bao lake la 26 msimu huu

Man City imepanda kileleni mwa msimamo wa ligi kwa tofauti ya mabao dhidi ya Arsenal huku timu zote zikiwa na alama 51

Arsenal wana mechi moja ya kiporo dhidi ya Aston Villa ambapo kama watashinda basi watarejea tena katika nafasi yao

Hofu ya mashabiki wa Arsenal ni mwenendo wa timu yao kwani katika mechi tatu zilizopita wameambulia alama 1 tu

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
9h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
10h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
10h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
14h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
17h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
18h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
18h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
19h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
20h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
20h ago
READ MORE β†’