Transfer

Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi Februari 16 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
16 Feb 2023
Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi Februari 16 2023

Mmiliki wa Chelsea Todd Boehly amekutana na rais wa Paris St-Germain Nasser Al-Khelaifi mjini Paris kujadili uwezekano wa uhamisho wa mshambuliaji wa Brazil Neymar, 31, msimu wa joto. (Le Parisien - kwa Kifaransa)

Arsenal wanafuatilia hali ya mshambuliaji wa Manchester United Muingereza Marcus Rashford, 25, huku kukiwa na sintofahamu kuhusu kandarasi yake Old Trafford. (Football Insider)

Mkufunzi wa Arsenal Mikel Arteta ameitaka klabu hiyo kumsajili kiungo wa kati wa Uhispania Martin Zubimendi mwenye umri wa miaka 24 kutoka Real Sociedad. (Sport - kwa Kihispania)

Kocha wa Barcelona Xavi anasema kiungo wa Uholanzi Frenkie de Jong, 25, hakutaka kujiunga na Manchester United msimu uliopita wa joto, huku klabu hizo mbili zikitarajiwa kukutana kwenye Ligi ya Europa. (Sun)

Barca wamefikia mkataba na LA Galaxy kumsajili beki wa Mexico Julian Araujo, 21, hadi Juni 2026. (Fabrizio Romano)

Araujo atawasili Barcelona siku ya Alhamisi kuanza mazoezi na mabingwa hao wa Uhispania. (ESPN)

Tottenham wanavutiwa na mlinzi wa Ecuador Piero Hincapie mwenye umri wa miaka 21 kutoka Bayer Leverkusen. (Caught Offside)

Aston Villa inaweza kusikiliza ofa kwa mlinda mlango wa Argentina Emiliano Martinez, 30, ili kusaidia kufadhili ujenzi wa klabu hiyo msimu wa joto. (Barua)

Beki wa Ureno Joao Cancelo, 28, anasema tetesi kwamba alitofautiana na mkufunzi wa Manchester City Pep Guardiola kabla ya uhamisho wake wa mkopo kwenda Bayern Munich ni uongo (Mundo Deportivo, via Mirror)

Mauricio Pochettino anaweza kurejea kama meneja wa Tottenham na kuchukua nafasi ya Antonio Conte. (TalkSPORT)

Chelsea, Liverpool, Manchester City, Manchester United na Newcastle zimewasiliano na klabu ya Independiente del Valle ya Ecuador kumhusu kiungo wa kati Kendry Paez, 15. (90min)

BBC

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
8h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
8h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
8h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
12h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
15h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
16h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
16h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
17h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
18h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
19h ago
READ MORE β†’