Kamwe amtetea beki mpya Yanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 16th February 2023


Kamwe amtetea beki mpya Yanga

Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amewatoa hofu wapenzi na wanachama wa klabu hiyo kuwa ni suala la muda tu watamuona beki wao mpya Mamadou Doumbia

Tangu alipotua Yanga kwenye usajili wa dirisha dogo, Doumbia aliitumikia Yanga kwa takribani dakika 30 kwenye mchezo wa kombe la FA dhidi ya Rhino Rangers

Kamwe amesema Doumbia anaendelea kuzoeana na wenzake katika viwanja vya mazoezi na Kocha Mkuu wa Yanga Nasreddine Nabi amesema nyota huyo yuko tayari

"Kocha Nabi ameridhishwa na maendeleo yake mazoezini, nafikiri ni suala la muda tu mashabiki watamuona uwanjani. Doumbia ni beki mzuri sana Mwalimu alihakikisha anamuandaa vizuri kuepuka kuathiri muunganiko ambao tayari ametengeneza pale kwenye safu ya ulinzi," alisema Kamwe

Baada ya kuruhusu mabao mawili ya aina moja kwenye mchezo dhidi ya US Monastir, kumekuwa na midajala miongoni mwa mashabiki wa Yanga huku wengine wakihoji kwa nini Doumbia hatumiki

Beki huyo mrefu alikuwa nahodha wa kikosi cha timu ya Taifa ya Mali kilichoshiriki michuano ya CHAN huko Algeria


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.