Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Raja Casablanca ambao utapigwa kesho Jumamosi katika uwanja wa Benjamin Mkapa, saa 1 usiku
AKizungumza katika mkutano na wanahabari leo, Robertinho alisema anatambua wanakwenda kupambana na timu kubwa lakini hata Simba ni kubwa pia
Amesema jukumu la wachezaji wake ni kucheza kwa malengo na kufuata maelekezo, wanayo nafasi ya kushinda mchezo huo
"Ni mechi ngumu, Raja Casablanca ni timu kubwa kama tulivyo sisi, lakini tuna malengo. Kutokana na mipango yetu, tumejipanga kushinda"
"Tuna malengo ya kuvuka hatua ya makundi kwenda robo fainali, nusu fainali na hata kutwaa ubingwa inawezekana. Nimewaandaa vijana wangu kucheza soka safi ambalo litaambatana na ushindi," alisema Robertinho
Akizungumzia kukosekana kwa kiungo mkabaji Sadio Kanoute anayetumikia adhabu ya kadi tatu za njano, Robertinho amesema kukosekana kwa mchezaji huyo hakutaathiri kikosi chake
"Tutamkosa Sadio Kanoute lakini sina wasiwasi kwa sababu timu yangu ina wachezaji wengi. Hatuchezi kumtegemea mchezaji mmoja, nawaamini wachezaji 11 watakaonza watatupa matokeo ya ushindi"