Jitihada za Ruvu Shooting kujinusuru na hatari ya kushuka daraja zimekumbana na dhoruba huko Nyankumbu Geita baada ya kukubali kipigo cha mabao 3-2 kutoka kwa Geita Gold
Ulikuwa mchezo mzuri wenye ushindani mkali Geita Gold wakiendeleza ubabe wao katika uwanja wa nyumbani
Bashina Sayte, Geofrey Manyasi na Elias Maguli walifunga mabao ya Geita wakati Shaban Mgandila na Abdulrahman Mussa wakifunga mabao ya Ruvu
Geita Gold imeendelea kubaki nafasi ya tano katika msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama 34 wakati Ruvu wanabaki nafasi ya 15 wakiwa na alama 17 alama moja mbele ya Polisi Tanzania inayoburuza mkia ikiwa na alama 16




