Transfer

Tetesi za soka Ulaya, Jumatatu Februari 20 2023

Joel JJ By Joel JJ
20 Feb 2023
Tetesi za soka Ulaya, Jumatatu Februari 20 2023

Bayern Munich wameungana na Paris St-Germain katika mbio za kumsajili winga wa Chelsea na Morocco Hakim Ziyech, 29. (Fijaches - in Spanish)

Mlinzi wa kati wa RB Leipzig na Croatia Josko Gvardiol, 21, anasema anataka kucheza katika Ligi ya Premia na alikuwa karibu kujiunga na Leeds United mnamo 2020 na karibia angesajiliwa na Chelsea msimu uliopita wa joto. (Times – Subscription Required)

Mmiliki wa Chelsea Todd Boehly hana nia ya kumfuta kazi meneja Graham Potter licha ya kushindwa kwa The Blues 1-0 na Southampton Jumamosi. (Mirror)

Barcelona wanamfuatilia kwa karibu kiungo wa kati wa Manchester City na Uhispania Rodri kabla ya dirisha la majira ya joto na watakuwa tayari kutoa pauni milioni 80 kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26. (Football Insider)

Tottenham wanamtaka meneja wao wa zamani Mauricio Pochettino kama mbadala wa Antonio Conte ikiwa Muitaliano huyo ataondoka Spurs mwishoni mwa msimu huu. (Nicolo Schira)

Newcastle United inamfuatilia kwa karibu beki wa Arsenal na Scotland Kieran Tierney, 25. (Football Insider)

Familia ya Glazer imepewa usaidizi wa kifedha wa kusalia kama wamiliki wa Manchester United na Uongozi wa Hedge fund wa Marekani Elliott baada ya kikundi hicho chenye makao yake makuu mjini New York kusajili nia ya kuwekeza katika klabu hiyo. (ESPN)

Inter Milan ndio walio mstari wa mbele kumsajili mshambuliaji wa Borussia Monchengladbach na Ufaransa Marcus Thuram, 25, mbele ya Manchester United na Bayern Munich. (Calciomercato – in Itali )

Chelsea na Tottenham wanafikiria kumnunua mshambuliaji wa Brighton wa Jamhuri ya Ireland Evan Ferguson, 18. (Sun)

Sevilla wana nia ya kupata mkataba wa mkopo kwa beki wa pembeni wa Manchester City Mhispania Sergio Gomez, 22. (Fijaches - in Spanish)

BBC

More Stories

SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
17m ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
1h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
12h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
12h ago
READ MORE →
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
12h ago
READ MORE →
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
16h ago
READ MORE →
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
19h ago
READ MORE →
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
20h ago
READ MORE →
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
21h ago
READ MORE →
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
21h ago
READ MORE →