KMC - Yanga - Azam

Yanga, Azam Fc zaitega KMC Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
20 Feb 2023
Yanga, Azam Fc zaitega KMC Ligi Kuu

Timu ya KMC imejikuta katika wakati mgumu kutokana na kuwa na mechi ngumu mfululizo dhidi ya Yanga na Azam huku ikiwa katika nafasi ya 12 ya msimamo wa Ligi Kuu Bara

KMC ambayo ipo nafasi ya 12 ikiwa na alama 23, Jumatano inatarajia kuvaana na Yanga huku Jumamosi wiki hii ikishuka dimbani dhidi ya Azam FC ambayo na yenyewe inawania angalau kumaliza nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara.

Afisa Habari wa KMC, Christina Mwagala, amesema kipindi walichonacho kwa sasa ni kigumu kutokana na kukabiliwa na michezo migumu dhidi ya Yanga na Azam zote zikiwa zinawania nafasi za juu.

"Mechi yetu na Yanga itakuwa ngumu kwa kuwa wao wapo katika presha ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu na mashindano ya kimataifa, pia wanaongoza kwenye msimamo, hivyo wanahitaji kupata matokeo mazuri"

"Pia ukiangalia wamepishana pointi sita na wapinzani wao, Simba hivyo, watahitaji ushindi ili wasipoteze pointi kwa kupata alama tatu," alisema na kuongeza:

"Ukiangalia katika kipindi hiki, KMC inapitia wakati mgumu zaidi ya vipindi vyote kwani Jumatano tunacheza na Yanga kisha Jumamosi tunacheza na Azam ambayo inahitaji kujiweka vizuri, mechi zote ngumu huku tukiwa nafasi ya 12"

"Ukiachana na michezo hiyo wanaotufuatia nyuma wanapambana ili na wao waweze kuja juu, lakini tumejipanga kufanya vizuri na hali ya kikosi ipo vizuri wachezaji wetu ambao walikuwa majeruhi wamerejea kwa ajili ya kupambana ili kumaliza katika nafasi nzuri," alisema Mwagala.

Yanga ipo kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo ikiwa na alama 59, ikifuatiwa na Simba yenye pointi 53, zote zikiwa zimecheza mechi 22, huku Singida Big Stars iliyopo nafasi ya tatu yenyewe na alama 44 ilizozipata kwa kushuka dimbani mara 23.

Azam FC iliyoshuka dimbani mara 22, yenyewe ipo nafasi ya nne ikiwa na pointi 43, jambo ambalo linaongeza ushindani kati yao na Singida Big Stars kuwania kumaliza nafasi ya tatu

IPP Media

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
7h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
7h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
7h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
11h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
14h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
15h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
16h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
16h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
17h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
18h ago
READ MORE β†’