Hersi ateta na Kinzumbi, amshawishi atue Yanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 21st February 2023


Hersi ateta na Kinzumbi, amshawishi atue Yanga

Juzi baada ya mchezo wa kombe la Shirikisho kati ya Yanga dhidi ya TP Mazembe uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa na Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 3-1, Rais wa Yanga Injinia Hersi Said alionekana akiteta na winga hatari wa TP Mazembe Fellipe Kinzumbi

Kinzumbi anayetumia mguu wa kushoto alikuwa mwiba kwa safu ya ulinzi ya Yanga kwani ndiye mchezaji aliyeonekana kuisumbua ngome ya Yanga iliyokuwa chini ya nahodha Bakari Nondo Mwamnyeto

Baada ya mchezo, Hersi alionekana akimpongeza nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 lakini pia akawa na mazungumzo nae ya faragha kwa muda mfupi

Moja ya mkakati wa Yanga kuelekea msimu ujao ni kuimarisha safu yake ya mawinga ambayo msimu huu imekuwa haina nguvu kubwa

Hersi anafahamika kwa kuwa na ushawishi mkubwa kwa wachezaji kutoka DR Congo, mpaka sasa Yanga ikiwa na wachezaji sita kutoka nchini humo

Mwanzoni mwa msimu huu Kinzumbi alikuwa na mgogoro na mabosi wake TP Mazembe akiwatuhumu kutaka kuongeza muda wa mkataba wake pasipo makubaliano


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.