Mlinda lango namba mbili wa Simba Beno Kakolanya yuko mbioni kusaini mkataba mpya kuendelea kuwatumikia wekundu hao wa Msimbazi, imefahamika
Kakolanya ni miongoni mwa wachezaji ambao mikataba yao inamalizika mwishoni mwa msimu huku kukiwa na taarifa za kipa huyo kuwaniwa na timu nyingine pia
Ukizungumzia makipa bora Watanzania, baada ya Manula anayefuatia ni Kakolanya
Habari za uhakika kutoka ndani ya uongozi wa Simba tayari mabosi wa Simba chini ya Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Salim Abdallah 'Try Again' wameanza nae mazungumzo ili kuhakikisha anasaini mkataba mpya kabla ya msimu kumalizika
Kakolanya amekuwa na wakati mzuri tangu aliposajiliwa na Simba akitokea klabu ya Yanga. Msimu huu amefanya vizuri katika mechi zote alizoanza kikosi cha kwanza