Geita Gold

Geita Gold kusajili Wanachama kidigitali

Joel JJ By Joel JJ
21 Feb 2023
Geita Gold kusajili Wanachama kidigitali

Klabu ya soka ya Geita Gold imezindua rasmi mfumo wa kusajili wanachama kidigitsli

Akizungumza leo katika mkutano na wanahabari Katibu mtendaji wa klabu Saimon Shija amesema kwa mujibu wa katiba ya klabu hiyo ibara ya 5 inawatambua wanachama kama sehemu ya kuiongoza klabu na kufanya maamuzi.

"Licha ya kuwa klabu inamilikiwa na Halmashauri kwa kiwango kikubwa lakini katiba inatoa nafasi kwa wanachama kuwa sehemu ya umiliki"

Mwanachama atajiunga kwa kuchangia shilingi elfu 3 kwa Mwezi sawa na shilingi elfu 36 kwa mwaka na atasajiliwa katika mfumo maalumu wa wanachama kwa utaratibu ulioweka na klabu.

Aidha Mwanachama baada ya kusajiliwa atapokea kadi yake ya uachama iliyo katika mtindo wa kidigitali

"Kwa kuzingatia pia kuwa tunawachama na mashabiki kutoka pande zote za Tanzania tumezindua namba Maalumu ya kuchangia na kulipia ada ya uachama ya LIPA NAMBA 5215290 GEITA GOLD FOOTBALL CLUB

"Klabu imekusudia kupokea wanachama wasiopungua elfu 2 kwa Mwaka kama sehemu ya kuimarisha timu. Aidha mpango huu wa kusajili wanachama ni endelevu na tutafanya jitihada kubwa kuimarisha mfumo huu na kuwa na klabu yenye ukubwa na ushindani lakini pia kuongeza nguvu ya kiuchumi ndani ya klabu"

More Stories

Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
40m ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
2h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
3h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
4h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
4h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
4h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
4h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
4h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
6h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
16h ago
READ MORE →