Katika kuhakikisha wanapata sapoti ya kutosha katika mchezo wa ligi ya mabingwa ambao watacheza siku ya Jumamosi dhidi ya Vipers Fc huko Uganda, klabu ya Simba imewapa fursa mashabiki wake kusafiri na timu
Simba inahitaji kushinda mechi zote mbili (ugenini na nyumbani) dhidi ya Vipers Fc ili kufufua matumaini ya kutinga robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika
Msafara wa mashabiki unatarajiwa kuondoka siku ya Alhamisi na kurejea Jumapili baada ya mchezo dhidi ya Vipers Fc




