Transfer

Tetesi za soka Ulaya, Jumatano Februari 22 2023

Joel JJ By Joel JJ
22 Feb 2023
Tetesi za soka Ulaya, Jumatano Februari 22 2023

Kiungo wa kati wa Chelsea N'Golo Kante, 31, anatazamiwa kusaini mkataba mpya na klabu hiyo huku mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa akikaribia kurejea kutokana na jeraha. (Telegraph – Subscription Required)

Aston Villa wako tayari kusikiliza ofa kwa mlinda mlango Emiliano Martinez, 30, ambaye aliisaidia Argentina kushinda Kombe la Dunia mwaka jana. (Mail)

Manchester United haitarajiwi kubadilisha uhamisho wa mkopo wa mshambuliaji wa Uholanzi Wout Weghorst mwenye umri wa miaka 30 kutoka Burnley kuwa uhamisho wa kudumu wakati wa dirisha la usajili la majira ya kiangazi. (Football Insider)

Leicester City wanajaribu kumshawishi kiungo mchezeshaji James Maddison kusaini mkataba mpya, lakini watataka kumuuza mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 msimu wa joto ikiwa haitaonekana kama atasalia katika klabu hiyo.

Manchester City, Newcastle United na Tottenham wanavutiwa na mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza. (Football Insider)

Meneja wa Brighton Roberto de Zerbi, 43, anavutia vilabu vikuu katika nchi yake ya Italia, huku pia akihusishwa na Tottenham. (Telegraph - usajili unahitajika)

Winga wa Crystal Palace Wilfried Zaha, 30, amekataa ofa nyingi za kuongeza kandarasi yake ya Eagles na klabu ya Al Nassr, ambayo ilimsajili fowadi wa Ureno Cristiano Ronaldo, 38, ni miongoni mwa klabu tatu za Saudi Arabia ambazo zimemtaka mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast. (Evening Standard)

Mtaalamu wa lishe wa Al Nassr Jose Blesa anasema wachezaji wote wanafanya mazoezi kwa bidii na kufuata mpango wa lishe tangu kuwasili kwa Ronaldo. (Ideal, via Mirror)

Arsenal wanatayarisha ofa ya kumnunua mshambuliaji wa Atalanta na Denmark Rasmus Hojlund, 20. (La Repubblica – in Italian)

Mshambulizi wa Napoli na Nigeria Victor Osimhen, 24, hajakataa kuondoka katika klabu hiyo ya Italia msimu huu wa joto na anasema kuvutiwa na vilabu vikubwa vya Ulaya kunatoa motisha ya ziada ya kucheza vyema kwa ajili yake na timu yake. (ESPN)

Leeds United wanapanga kumnunua mshambuliaji wa Sweden Viktor Gyokeres, 24, ambaye mkataba wake na Coventry City utaendelea hadi majira ya joto 2024. (Teamtalk).

Kiungo wa kati wa Urusi Arsen Zakharyan, 19, hatahamia Galatasaray kutoka Dynamo Moscow, licha ya timu hiyo ya Uturuki kumtaka. (Fabrizio Romano)

BBC

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
12h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
13h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
15h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
15h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
16h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
16h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
17h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
17h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
17h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
19h ago
READ MORE →