Real Madrid ilitokea nyuma na kupata ushindi wa mabao 5-2 dhidi ya Liverpool katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa hatua ya 16 bora Ligi ya mabingwa barani Ulaya
Wenyeji Liverpool walifunga bao la kwanza kwenye Uwanja wa Anfield Darwin Nunez akimchambua kipa wa Real Madrid Thibaut Courtois
Wakionekana kuwa katika ubora mkubwa, Liverpool wakaongeza la pili katika dakika ya 14 baada ya Mohamed Salah kutumia makosa ya mlinda lango Courtois
Hata hivyo Real Madrid walirejea mchezoni ambapo Dakika ya 21 Vinicius Junior aliifungia Real Madrid bao la kwanza
Vinicius tena akafanya matokeo kuwa 2-2 katika dakika ya 36 akitumia makosa ya mlinda lango Alisson
Wageni Real Madrid walirejea kipindi cha pili wakiwa wa moto kwelikweli, Mbrazil Eder Militao akaongeza bao la tatu kabla ya Karimu Benzema kuongeza mecngine mawili
Liverpool wamejiweka katika nafasi ngumu ya kutinga robo fainali kwani sasa watahitaji kupata ushindi huko Hispania
Lakini matokeo haya yanaweza yasiwashangaze mashabiki wa Liverpool kutokana na mwenendo wa timu yao msimu huu
Katika mchezo mwingine uliopigwa jana, Eintracht Frankfurt walikubali kipigo cha mabao 2-0 nyumbani dhidi ya timu bora kwa wakati huu barani Ulaya, Napoli



