Liverpool hoi mbele ya Real Madrid

Joel JJ By Joel JJ β€’ 22nd February 2023


Liverpool hoi mbele ya Real Madrid

Real Madrid ilitokea nyuma na kupata ushindi wa mabao 5-2 dhidi ya Liverpool katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa hatua ya 16 bora Ligi ya mabingwa barani Ulaya

Wenyeji Liverpool walifunga bao la kwanza kwenye Uwanja wa Anfield Darwin Nunez akimchambua kipa wa Real Madrid Thibaut Courtois 

Wakionekana kuwa katika ubora mkubwa, Liverpool wakaongeza la pili katika dakika ya 14 baada ya Mohamed Salah kutumia makosa ya mlinda lango Courtois

Hata hivyo Real Madrid walirejea mchezoni ambapo Dakika ya 21 Vinicius Junior aliifungia Real Madrid bao la kwanza

Vinicius tena akafanya matokeo kuwa 2-2 katika dakika ya 36 akitumia makosa ya mlinda lango Alisson

Wageni Real Madrid walirejea kipindi cha pili wakiwa wa moto kwelikweli, Mbrazil Eder Militao akaongeza bao la tatu kabla ya Karimu Benzema kuongeza mecngine mawili

Liverpool wamejiweka katika nafasi ngumu ya kutinga robo fainali kwani sasa watahitaji kupata ushindi huko Hispania

Lakini matokeo haya yanaweza yasiwashangaze mashabiki wa Liverpool kutokana na mwenendo wa timu yao msimu huu

Katika mchezo mwingine uliopigwa jana, Eintracht Frankfurt walikubali kipigo cha mabao 2-0 nyumbani dhidi ya timu bora kwa wakati huu barani Ulaya, Napoli


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.