Transfer

Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi Februari 23 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
23 Feb 2023
Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi Februari 23 2023

Arsenal wako tayari kumenyana na Borussia Dortmund, Newcastle na Juventus kuwania saini ya beki wa kulia wa Real Valladolid raia wa Uhispania Ivan Fresneda, 18. (Standard)

Kipa wa England Jordan Pickford, 28, anakaribia kusaini mkataba mpya na Everton. (Times - subscription required)

Arsenal pia wameanza mazungumzo ya kuongeza mkataba na kiungo wa kati wa Uswizi Granit Xhaka, 30, ambaye ana nia ya kusalia Emirates Stadium. ( 90,min)

Liverpool wanavutiwa na mlinzi wa RB Leipzig na Croatia Josko Gvardiol, 21. (Fabrizio Romano)

Beki wa Ureno Joao Cancelo, 28, anasema uhamisho wake wa mkopo kwenda Bayern Munich ilikuwa fursa ambayo hangeweza kuikataa baada ya kuamini kwamba anafaa kucheza zaidi Manchester City, huku meneja Pep Guardiola akipinga. (O Jogo, via Mail)

Mkurugenzi wa Shakhtar Donetsk Darijo Srna anasema klabu hiyo itajaribu kumsajili tena fowadi wa Ukraine mwenye umri wa miaka 22 Mykhailo Mudryk siku zijazo baada ya kuhamia Chelsea mwezi uliopita. (Football Ramble, via Football.london)

Ajenti wa kiungo wa kati wa Austria Marcel Sabitzer amedokeza kwamba mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 anaweza kusalia Manchester United hadi mwisho wa msimu huu kufuatia uhamisho wake wa mkopo kutoka Bayern Munich. (Sport 1 – In Germany )

Rais wa Napoli Aurelio de Laurentiis ameipa Manchester United matumaini ya kumsajili mshambuliaji wa Nigeria Victor Osimhen, 24, baada ya kusema "wakati mwingine kuna ofa ambazo huwezi kukataa". (Mirror)

Leicester City wanaweza kutafuta kumsajili kiungo wa kati wa Borussia Dortmund na Ujerumani Mahmoud Dahoud, 27, kwa uhamisho wa bila malipo msimu wa joto. (Leicester Mercury)

Kipa wa zamani wa England Ben Foster, 39, anasema hajutii kukataa nafasi ya kustaafu na kusaini Newcastle, ambayo kipa wake chaguo la kwanza Nick Pope amepigwa marufuku kwa fainali ya Kombe la Carabao Jumapili. (TalkSPORT)

BBC

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
2m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
31m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’