Bao la Tariq Seif liliihakikishia Mbeya City ushindi muhimu wa bao 1-0 dhidi ya Polisi Tanzania katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa uwanja wa Sheikh Amri Abeid
Polisi Tanzania walikuwa wenyeji wa mchezo huo ambao ulihamishwa kutoka uwanja wa Ushirika kutokana na uwanja huo kuwa na matumizi mengine
Sio matokeo mazuri kwa Polisi Tanzania ambayo inashika nafasi ya 15 kwenye msimamo wa ligi
Kocha Mkuu wa Polisi Tanzania Mwinyi Zahera amesema licha ya kipigo hicho hawawezi kukata tamaa, bado kuna mechi sita za kupambana ili kubaki ligi kuu
Kocha Mkuu wa Mbeya City Abdallah Mubiru amesema ni alama tatu muhimu kwao zilizowafanya wafikishe alama 27
Mubiru amesema malengo yao ni kuona wanamaliza katika nafasi tano za juu kwenye msimamo
Wanahitaji kupata angalau alama 10 kutoka mechi sita zilizosalia kuhitimisha msimu huu



