Polisi Tanzania chali mbele ya Mbeya City

Joel JJ By Joel JJ β€’ 23rd February 2023


Polisi Tanzania chali mbele ya Mbeya City

Bao la Tariq Seif liliihakikishia Mbeya City ushindi muhimu wa bao 1-0 dhidi ya Polisi Tanzania katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa uwanja wa Sheikh Amri Abeid

Polisi Tanzania walikuwa wenyeji wa mchezo huo ambao ulihamishwa kutoka uwanja wa Ushirika kutokana na uwanja huo kuwa na matumizi mengine

Sio matokeo mazuri kwa Polisi Tanzania ambayo inashika nafasi ya 15 kwenye msimamo wa ligi

Kocha Mkuu wa Polisi Tanzania Mwinyi Zahera amesema licha ya kipigo hicho hawawezi kukata tamaa, bado kuna mechi sita za kupambana ili kubaki ligi kuu

Kocha Mkuu wa Mbeya City Abdallah Mubiru amesema ni alama tatu muhimu kwao zilizowafanya wafikishe alama 27

Mubiru amesema malengo yao ni kuona wanamaliza katika nafasi tano za juu kwenye msimamo

Wanahitaji kupata angalau alama 10 kutoka mechi sita zilizosalia kuhitimisha msimu huu


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.