Yanga

Doumbia, Diarra kuibeba Yanga Mali?

Joel JJ By Joel JJ
24 Feb 2023
Doumbia, Diarra kuibeba Yanga Mali?

Wananchi wako Mali ambapo Jumapili jioni watashuka Stade du 26 Mars kuikabili Real Bamako katika mchezo wa raundi ya tatu hatua ya makundi kombe la Shirikisho barani Afrika

Kwa mara ya kwanza nyota wawili wa Yanga Mamadou Doumbia na Djigui Diarra wanarejea Mali lakini sasa wakibeba ramani ya ushindi wa Yanga dhidi ya timu ya nyumbani kwao

Doumbia alisajiliwa na Yanga dirisha dogo, lakini bado hajaingia kwenye kikosi cha kwanza cha kocha Nasreddine Nabi

Ni mchezaji mwenye uzoefu mkubwa na soka la Mali, alikuwa nahodha wa kikosi cha Mali kilichokwenda kushiriki michuano ya CHAN nchini Algeria

Ni wazi Nabi huenda akamtumia katika mchezo huo kama ilivyo kwa Djigui Diarra kutokana na uzoefu wao na soka la Mali

Real Bamako sio wepesi licha ya kupoteza mchezo wa kwanza ugenini kwa kufungwa mabao 3-1 na TP Mazembe na kisha kulazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya US Monastir nyumbani

Tayari wamedondosha alama mbili nyumbani, wataweka nguvu kubwa zaidi katika mechi mbili zilizobaki nyumbani wakianza na mechi dhidi ya Yanga Jumapili

Alama moja kwa Yanga ugenini hayatakuwa matokeo mabaya lakini alama tatu yatakuwa matokeo bora zaidi ambayo yataiweka Yanga katika nafasi nzuri ya kutinga robo fainali

More Stories

SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
16m ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
1h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
12h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
12h ago
READ MORE →
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
12h ago
READ MORE →
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
16h ago
READ MORE →
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
19h ago
READ MORE →
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
20h ago
READ MORE →
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
21h ago
READ MORE →
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
21h ago
READ MORE →