Simba iko nchini Uganda ambapo leo majira ya saa 1 usiku itashuka uwanja wa St Marry's Kitende kuwakabili wenyeji wao Vipers Fc katika mchezo wa raundi ya tatu michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika
Mechi muhimu sana kwa Simba nchini Uganda, kwani dakika 90 za mchezo huo zitaamua hatma, malengo ya Simba katika michuano hiyo msimu huu
Baada ya kupoteza mechi mbili za kwanza, kimahesabu Simba bado ina alama 12 za kuwania mezani, ushndi utarudisha matumaini ya kusonga ya kwenda hatua ya robo fainali kwani Simba bado itakuwa na mechi mbili nyumbani ambazo kama watashinda watakuwa na uhakika wa kukusanya alama tisa kabla ya mechi ya mwisho dhidi ya Raja ambayo itapigwa Morocco
Lakini matokeo tofauti na ushindi yatafifisha matumaini hayo ya Wekundu wa Msimbazi, watahitaji muujiza kuweza kutinga robo fainali
Hivyo mechi ya leo ni moja kati ya zile mechi kubwa ambazo Simba ilihitaji kucheza kibingwa kuweza kuibuka na ushindi
Simba imekuwa na rekodi nzuri kwenye mechi za ugenini katika michuano ya ligi ya mabingwa msimu huu
Walishinda mechi zote za ugenini kwenye raundi za awali dhidi ya Nyasa Big Bullets na Primero De Agosto na kama wachezaji wangekuwa makini, wangepata matokeo mazuri katika mchezo wa kwanza wa makundi dhidi ya Horoya Ac ambao walipoteza kwa bao 1-0
Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amesema wanatambua mchezo huo utakuwa mgumu sana lakini wako Uganda kusaka ushindi
Kabla ya kutua Simba, Robertinho alikuwa akiinoa Vipers Fc hivyo anawafahamu vyema na leo kazi itakuwa moja tu kwa Simba, KUWAPIGA