Potter na familia yake watishiwa maisha

Joel JJ By Joel JJ β€’ 25th February 2023


Potter na familia yake watishiwa maisha

Kocha wa Chelsea, Graham Potter amefichua kuwa alipokea vitisho vya kuuawa, lakini amesisitiza haikumuathiri kisaikolojia kwani analenga kubadilisha mwenendo wa klabu.

Potter alisema kuwa alishambuliwa kwa njia ya barua pepe baada ya mfululizo wa matokeo mabaya 

"Kama vile nimekuwa nikiungwa mkono nimekuwa na barua pepe zisizo nzuri sana ambazo zilinitaka kufa na kutaka watoto wangu wafe, kwa hivyo ni wazi kwamba hiyo haipendezi," alisema Potter

Potter yuko kwenye presha kubwa Stamford Bridge kufuatia kichapo cha 1-0 Jumamosi iliyopita dhidi ya Southampton inayoshika mkia kwenye Ligi Kuu ya England.

Timu yake, ambayo inashika nafasi ya 10 kwenye ligi, imeshinda mara mbili pekee katika michezo 14 iliyopita na imefunga bao moja nyumbani mnamo 2023.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.