Yanga

Yanga yapata alama moja muhimu Mali

Joel JJ By Joel JJ
β€’
26 Feb 2023
Yanga yapata alama moja muhimu Mali

Yanga imefanikiwa kuondoka na alama moja nchini Mali baada ya kulazimisha sare ya bao 1-1 dhidi ya Real Bamako katika mchezo wa raundi ya tatu, kundi D Kombe la Shirikisho barani Afrika

Yanga ilikuwa bora kwa muda mwingi wa mchezo na hakika matokeo haya wachezaji hawawezi kuyafurahia kwa sababu walikaribia kuondoka na alama zote tatu

Fiston Mayele alifunga bao la Yanga kwenye dakika ya 60 baada ya pasi murua kutoka kwa Stephane Aziz Ki

Hata hivyo kukosekana kwa umakini katika kucheza mpira wa kona kuliigharimu Yanga kwenye dakika ya 90 Real Bamako wakisawazisha bao hilo kupitia kwa Emile Kone

Yanga inarejea Dar na alama moja muhimu ambayo imeendelea kuwaweka kwenye nafasi ya pili wakifikisha alama nne nyuma ya US Monastir wenye alama saba

Mapema Monastir waliichapa TP Mazembe mabao 2-0 katika mchezo uliopigwa DR Congo

Yanga na Real Bamako zitakipiga tena uwanja wa Benjamin Mkapa Machi 08

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
9h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
9h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
9h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
13h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
16h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
17h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
17h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
18h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
19h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
20h ago
READ MORE β†’