Yanga imefanikiwa kuondoka na alama moja nchini Mali baada ya kulazimisha sare ya bao 1-1 dhidi ya Real Bamako katika mchezo wa raundi ya tatu, kundi D Kombe la Shirikisho barani Afrika
Yanga ilikuwa bora kwa muda mwingi wa mchezo na hakika matokeo haya wachezaji hawawezi kuyafurahia kwa sababu walikaribia kuondoka na alama zote tatu
Fiston Mayele alifunga bao la Yanga kwenye dakika ya 60 baada ya pasi murua kutoka kwa Stephane Aziz Ki
Hata hivyo kukosekana kwa umakini katika kucheza mpira wa kona kuliigharimu Yanga kwenye dakika ya 90 Real Bamako wakisawazisha bao hilo kupitia kwa Emile Kone
Yanga inarejea Dar na alama moja muhimu ambayo imeendelea kuwaweka kwenye nafasi ya pili wakifikisha alama nne nyuma ya US Monastir wenye alama saba
Mapema Monastir waliichapa TP Mazembe mabao 2-0 katika mchezo uliopigwa DR Congo
Yanga na Real Bamako zitakipiga tena uwanja wa Benjamin Mkapa Machi 08








