Simba

Simba na hesabu kali robo fainali Ligi ya Mabingwa

Joel JJ By Joel JJ
27 Feb 2023
Simba na hesabu kali robo fainali Ligi ya Mabingwa

Baada ya kurejea kutoka Uganda ambako walifanikiwa kuichapa Vipers Fc bao 1-0 na kufufua matumaini ya kutinga robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika, kikosi cha Simba kinaanza maandalizi ya mechi mbili zinazofuata katika michuano hiyo ambazo zitapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa

March 07 Simba itaikaribisha Vipers Fc katika mchezo utakaopigwa saa 1 usiku kisha kufuatiwa na mchezo dhidi ya Horoya Ac ambao utapigwa March 18

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally amesema wanahitaji kuvuna alama zote sita katika mechi hizo mbili ambazo zitakuwa ngumu

"Asante Mungu Ushindi wetu wa Uganda ni ishara kuwa kazi ya kuitafuta robo fainali inaanza"

"Haitakua rahisi maana Vipers hatakubali kufungwa nje ndani na Horoya hatakubali kupoteza matumaini yake"

"Lakini yote yanawezekana kama kila Mwana Simba atatimiza majukumu yake. Agenda kuu ya Kitaifa ya Wana Simba hivi sasa ni Operation six points eye to the Quarter finals (Mpango ni alama 6 Jicho kwenye Robo Fainali)"

"Kila mwenye silaha, Mwenye mawazo na mwenye mbinu atumie ili azma yetu itimie Kwa mashabiki wenzangu tuanze sasa maandalizi ya March 7, Jukumu letu ni kuujaza Uwanja na kushangilia," aliandika Ahmed kwenye ukurasa wa mtandao wake wa kijamii

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
12h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
13h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
15h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
15h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
16h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
16h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
17h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
17h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
17h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
19h ago
READ MORE →