Transfer

Tetesi za soka Ulaya, Machi 1 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
1 Mar 2023
Tetesi za soka Ulaya, Machi 1 2023

Kocha wa Manchester United Erik ten Hag anataka kusajili angalau wachezaji wawili muhimu msimu huu wa joto, huku mshambuliaji wa Napoli na Nigeria Victor Osimhen, 24, na kiungo mshambuliaji wa Ajax Mghana Mohammed Kudus, 22, akiwa miongoni mwa malengo yake.(Manchester Evening News).

Kiungo wa kati wa Barcelona na Uholanzi Frenkie de Jong, 25, pia anasalia kulengwa na Manchester United msimu huu wa joto. (Sport - kwa Kihispania)

Manchester City wanafikiria kumnunua kiungo wa kati wa Croatia Mateo Kovacic msimu huu wa joto, wakati mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 atakuwa amebakiza mwaka mmoja kwenye mkataba wake Chelsea. (Telegraph - usajili unahitajika)

Beki wa Chelsea na Muingereza Ben Chilwell, 26, ni mchezaji mwingine anayelengwa na Manchester City msimu ujao. (Football Insider)

Klabu ya Borussia Dortmund na klabu ya zamani ya Naby Keita ya RB Leipzig zina nia ya kumsajili kiungo huyo wa kati wa Guinea, 28, mkataba wake wa Liverpool utakapokamilika msimu huu. (Bild - kwa Kijerumani)

Atletico Madrid wamekubaliana na beki wa Uturuki Caglar Soyuncu, 26, juu ya uhamisho wa bila malipo mkataba wake Leicester City utakapokamilika mwishoni mwa msimu huu. (90 Min)

Walengwa wakuu wa Real Madrid msimu huu wa joto ni Bellingham na beki wa RB Leipzig wa Croatia Josko Gvardiol, 21. (Sport - kwa Kihispania).

N'Golo Kante alikuwa na chaguo la kuondoka Chelsea kwa uhamisho wa bila malipo msimu huu lakini kiungo huyo wa kati wa Ufaransa, 31, anataka kusalia Stamford Bridge na anakaribia kuafikia mkataba mpya. (Fabrizio Romano)

BBC

More Stories

Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
34m ago
READ MORE β†’
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
10h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
11h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
11h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
14h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
18h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
19h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
19h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
20h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
20h ago
READ MORE β†’