Yanga - Taifa Stars - Tanzania

Nabi azima tetesi za kuinoa Stars

Joel JJ By Joel JJ
β€’
1 Mar 2023
Nabi azima tetesi za kuinoa Stars

Wakati uvumi ukienea kwamba Kocha Mkuu wa Yanga Nasreddine Nabi anawindwa kupewa kibarua cha kuwa kocha wa Timu ya Taifa 'Taifa Stars', mwenyewe ametoa hatma yake.

Nabi amesema kuwa anafurahia kupewa nafasi kubwa kama hiyo ya kuifundisha Taifa Stars lakini kwasasa ni vigumu kukubali ofa hiyo.

Nabi amesema kwasasa ajira pekee ambayo anaweza kuifanya akiwa ndani ya ardhi ya Tanzania ni kuendelea kuifundisha Yanga

"Nimeona hizo taarifa lakini hata familia yangu wameshtuka walipoona lakini niwashukuru wanaonifikiria kuhusu nafasi hiyo"

"Naomba waambie mashabiki wa Yanga kwamba mimi kwa hapa Tanzania kwasasa nitaifundisha timu yao pekee mpaka nitakapochukua uamuzi mwingine"

"Sina maana kwamba kuifundisha Tanzania ni kazi mbaya kwangu hapana lakini huwa nina utaratibu wa kumaliza jambo ambalo nimelianza," Nabi alinukuliwa na gazeti la Mwanaspoti

Tangu ajiunge na Yanga mwezi April 2021, Nabi ameisaidia timu hiyo kushinda mataji mawili ya ligi kuu na kombe la FA, Ngao mbili za jamii huku msimu huu akiiweka Yanga kileleni mwa msimamo wa ligi kwa tofauti ya alama nane

Huenda akawaongoza mabingwa hao watetezi kutetea ubingwa kwa msimu wa pili mfululizo

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
10h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
10h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
10h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
14h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
17h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
18h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
19h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
19h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
20h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
21h ago
READ MORE β†’